Huawei wasema wanategemea vifaa milioni 100 kutumia HarmonyOS kufikia mwisho wa mwaka huu. HarmonyOS ni programu endeshaji inayolenga kuleta ushindani kwa Android.
Makamu wa Rais wa Huawei, Bwana Xu Zhijun amesema kinachofanyika kwa sasa ni maboresho zaidi ya jinsi programu endeshaji hiyo inatambua na kufanya kazi kwa ufanisi kwenye vifaa vya elektroniki vya aina tofauti tofauti. Ni lengo la Huawei kuiwezesha programu endeshaji hii kutumika kwenye vifaa vingi tofauti kama vile Televesheni janja, simu janja, saa janja, na vifaa vingine mbalimbali vya elektroniki vya kisasa.
Huawei wamesema hadi sasa programu endeshaji hiyo imeshapata makampuni 20 ya utengenezaji vifaa yaliyoonesha nia ya utumiaji wa HarmonyOS. Pia tayari kuna makampuni 280 ya utengenezaji apps ambayo tayari yameomba ushirikishwaji wa karibu katika utengenezaji wa programu endeshaji hiyo.
Huawei wamesema wanategemea watumiaji wa simu za Huawei za kisasa kama vile mate X2 waweze kusasisha na kupata HarmonyOS kwenye simu zao kufikia mwezi Aprili hadi Juni mwaka huu.
No Comment! Be the first one.