Kitu chocohote kile kizuri unachokifanya halafu ikatokea ukapongezwa kwa namna yoyote ile hakika inaletaa furaha na hamaasa ya kuendelea kufanya vizuri zaidi ndivyo hivyo Samsung wamefanikiwa kunyakua jumla ya tuzo 71 za iF Design Awards mwaka 2021.
Samsung Electronics ambayo hakuna asiyeijua duniasni kote hivi karibuni imewafikiwa kuwafurahisaha jopo la majaji mara 71 kwenye tuzo za “iF Design Awards“. Tuzo hizi za iF Design Awards ni mahususi kwa ajili ya kutathimini muundo vitu mbalimbali vya kidijiti kwenye vipengele mbalimbali kama utalaamu wa uundaji, ufungaji, urahisi wa kutumia kitu, muundo wa ndani kwenye kitu husika, n.k. Tuzo hizo zimekuwa zikifanyika tangu mwaka 1953.
SAmdung ambao wameshinda jumla ya tuzo 71; 36 kati ya hizo zimetokana na bidhaa zao, 10 kwenye kipengele cha “Professional concept“, 11 kutoka kapu la “Communication designs“, 5 zikihusu “Packaging design” na 9 kutokana na kuvutia “User experience and interface“.
Bidhaa mbalimbali za Samsung zilizowezesha kushinda tuzo
Simu janja Samsung Galaxy Z Fold 2 na Z Flip ni miongoni mwa bidhaa zilishinda tuzo pamoja na runinga ya kisasa aina ya QLED 8K kutokana na muundo wa aina yake lakini pia ubora wa muonekano wa picha ndani runinga hizo.
Mbali na hilo bidhaa ya Samsung mahususi kwa ajili ya kuonyesha vitu kwenye ukuta, kitambaa/ubao mweupe, n.k kwa Kiswahili kirahisi tunasema projekta ni bidhaa nyingine iliyopeleka tuzo kwa Samsung Electronics baada ya kuwavutia majaji kutokana na muundo wake.
Ushindi huu ni mkubwa na kuweka alama ya aina yake lakini pengine kuwafanya waendelee kutoa vitu vizuri na vya ushindani kweli kweli. Vipi unazungumziaje habari hii? Tunakaribisha maoni yako.
Vyanzo: GSMArena, Tovuti ya iF Design Awards
One Comment