Snapchat ni mtandao maarufu sana wa kijamii, licha ya kampuni kuwa inafanya vizuri na kufahmika sana bado inaonekana kuna shida kidogo katika mapato.
Ni sawa mapato yanapatikana na yanaongezeka tuu, ila sio kwa ile kasi ambayo ilikua inatarajiwa. Hii inamaana kwamba kama hali itaendelea hivi hivi ni ishara mbaya kwa kampuni.
Kama ikiendelea hivi pengine hata itawezekana mapato hayo kupungua kabisa, lakini kwa sasa Snapchat inaweza haijaridhika/haijapenda jinsi majibu ya makusanyo yao yalivyo.
Hii imeonekana katika taarifa za mapato zilizokusanywa za robo ya pili ya mwaka 2022, taarifa hizo zimeonekana kabisa kutoendana na matakwa ya kampuni hiyo.
Mapato yake katika robo ya pili ya mwaka ni dola bilioni 1.11 kumbuka mwishoni mwa mwaka 2021 yalikua ni dola milioni 982 na hata hivyo imeongeza watumiaji milioni 15.
Ningependa kusikia kutoka kwako, je unashauri ni nini kifanyike juu ya hili? Niandikie hapo chini katika sehemu ya comment.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.