Motorola itatambulisha vifaa hivi katika mkutano ambao umedhaminiwa kuwa ni utambulisho wa vifaa vyake ambao utakua ni mwezi agosti mwaka huu.
Pengine katika utambulisho huo ndio utaona simu ya kwanza kabisa yenye 200MP katika kamera yake.
Kwa majina vifaa hivyo ni Razr nyingine ikiwa ni muendelezo wa ile ya kwanza, huku kifaa kingine kikiwa ni Motorola X30 Pro
Kwa sasa inavyosemekana ni kwamba kwa matoleo ya simu hii ya Razr yatakua yanapatika huko china pekee, huku kampuni haijatoa tamko juu ya masoko mengine.
Kwa Motorola X30 Pro licha ya kuwa simu ya kwanza kuwa na 200MP lakini itakua na sifa zingine kama vile kioo cha nchi 6.67, chaja yake ina uwezo wa 125W (yenye uwezo wa kuchaji haraka Zaidi)
Cha kushangaa kidogo hapa ni kwamba nje ya soko la china simu hii itakua inajulikana kama Motorola Edge 30 Ultra
Ukija kwenye Razr ni kwamba itakua na vipengele ambavyo ni maboresho tuu kwa vipengele ambavyo vilipatikana katika Razr za nyuma
Vipengele kama display ya 120Hz, RAM 12GB, ujazo uhifadhi wa ndani ni 512GB kamera ni 50MP kwa 13MP huku kamera yake ya mbele (ya selfi) ni 32MP.
Soma Kila Kitu Kuhusu Motorola >>HAPA<<
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je uko tayari kuanza kutumia vifaa hivi? Vipi kuhusu upatikanaji wake?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.