Kama kitafanikiwa kipengele hichi kitakua na msaada mkubwa sana maana kwenda LIVE kupitia TikTok mambo mengi yanewza yakatokea mfano kama utumizi wa lugha mbaya n.k
Lakini kipengele hichi kinakijita sana katika kuhakikisha kuwa vijana wenye umri chini ya miaka 18 hawataweza kuonyeshwa video hiyo ya LIVE kama itakua sio ya maudhui yanayoendana na miaka hiyo.
Kinachotokea hapa ni kwamba kwa mtu ambae anaingia katika mtandao wa TikTok kwa lengo la kuingia LIVE basi kuna sehemu (mature theme) ambapo ukiwasha video yako haitaweza kuonekana na wale wenye umri chini ya miaka 18.
Pia unaweza ukakiwasha kipengele hichi hata kama katika kati ya video (yaani hukukiwasha tangia mwanzo) na kwa kufanya hvyo akaunti zote zenye umri chini ya miaka 18 zitatolewa katika video hiyo.
Kikibwa cha kufahamu hapa ni kwamba sio kwamba TikTok imekuja na kipengele hichi basi itakua imeruhusu maudhui ya kikubwa katika mtandao huo la-ha-sha.
Imefanya hivi uili kujiweka karibu na kufuata maadili katika jamii nah ii pia itasaidia waandaji wa maudhui katika kazi zao na kadhalika.
Kingine ni kwamba hii ni njia rahisi kabisa ya kutaka kujua kuwa ni maudhui gani mahususi kwa ajili ya watoto na wakubwa kwa mtandao.
Kipengele hichi hakitakoka wa watu wote kwa muda, nadhani baadae ndio kitasambaa kwa watu wote…
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je hii umeipokeaje? Unadhani hii ni njia sahihi ya kuilinda jamii?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.