Uamuzi wa kujitoa Umoja wa Ulaya unaifanya Uingereza kufikiria kila namna ambayo itawasaidia wao baada ya kukamilisha mchakato mzima wa kujiondoa kutoka kwenye umoja huo miezi kadhaa ijayo.
Mwaka 2003, Umoja wa Ulaya iliridhia ujenzi wa satelaiti kwa matumizi ya pamoja inayofahamiika kama Galileo ambayo inatarajiwa kukamilika mwaka 2020 na ikigharimu Euro 10bn|$11.44bn.
Satelaiti ya Galileo ikikamilika inatazamiwa kuwa mpinzani wa ile ya Marekani.
Kwanini Uingereza inataka kujenga satelaiti ya kwake mwenyewe?
Hatua hiyo imefuatia baada ya mpango wa Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya na kuelezwa kuwa kama nchi itaruhusiwa kutumia Galileo kupitia chaneli ya wazi lakini jeshi la nchi hiyo litadhibitiwa kwa kiwango fulani kuweza kutumia kifaa hicho huku tangu ujenzi wa satelaiti hiyo serikali ya Uingereza imechangia.
Sasa katika nia ya kuondoa mtafaruku kati ya Umoja wa Ulaya na Uingereza, kama nchi imeamua kujenga satelaiti ya kwake mwenyewe kwa ajili ya tafiti mbalimbali.
Pauni 100m zikiwa zimeidhinishwa kutoka Wizara ya Fedha kama sehemu ya gharama za ujenzi kifaa hicho.
Uingereza inatrgemea kudai fidia ya pauni 1bn iwapo Umoja wa Ulaya utaendelea kusisitiza kuibagua nchi hiyo mara baada ya kifaa hicho kuanza kufanya kazi.
Moja ya wataalam anaamini mpango huo wa Uingereza kujenga satelaiti ya kwao unaweza ukagharimu pauni 3bn mpaka kukamilika kwake.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|