Watumiaji wa iPhone ni wengi tuu duniani kwa maana ya kwamba simu hizo zinavutia wateja wengi ulimwenguni kiasi cha kuifanya Apple kuwa kampuni tajiri kuzidi yote kwenye soko la ushindani.
Nianze kwa kuuliza umeshawahi kutumia iPhone halafu kuna wakati inakukera kiasi kwamba unaanza kufiri juu ya kubadilisha pengine hata kuhamia upande wa Android? Binafsi nikiri kuwa kitu hicho kilishawahi kunitokea lakini ilinichukua muda mpaka kuja kufanya maamuzi ya kuweka kando iPhone.
Waswahili husema “Kizuri hakikosi kasoro”. Mtumiaji mmoja ambae pia ni mfanyakazi wa zamani wa Apple amejikuta akiachana kutumia iPhone na kuhamia Samsung baada ya changamoto ambayo imekuwa ikiwakumba watumiaji wengi wa simu janja husika kutopatiwa ufumbuzi licha ya msururu wa malalamiko ya watu kuhusiana na tatizo hilo lakini Apple wamekuwa wazito kulipatia ufumbuzi.
Taizo lenyewe ni kutoonekana kwa taarifa fupi mara tu zinapoingia au kuchelewa na kujitokeza baada ya muda fulani kwenye iOS 14. Kwa maneno yake anasema unaweza ukafikiri ni rahisi kuondoa tatizo hilo lakini lina ugumu wake. Amekuwa akifuatilia majadiliano ya Apple na watumiaji wake kupitia ukurasa maalum kabisa ya kuwasilisha matatizo. Tatizo hilo lipo pia kwenye saa janja za Apple zilizounganishwa na simu
Suala la changamoto mbalimbali zinazohusiana na taarifa fupi kwenye iPhone sasa zinakaribia kurasa 100 za maswali/majibu kati ya Apple na watumiaji wake. Sasa ili kuepukana na kdhia hiyo mfanyazi huyo wa zamani wa Apple akaamua kutumia simu janja ya Samsung.
Waswahili husema “Kheri nusu shari kuliko shari kamili”. Tuambie ingekuwa ni wewe umepatwa na changamoto hiyo ungefanyaje? Tunakaribisha mawazo yako na endelea kutufuatilia kila siku.
Vyanzo: ZDNet, Piunika Web
No Comment! Be the first one.