Snapchat ni mtandao wa kijamii ambao ulikuja kwa kasi sana, ukiachana na ujuo wake huo bado ilianza kushuka kwa haraka ikawa kinyume cha watu walivyodhania. Kabla ya isntagram, WhatsApp na Facebook hazijaja na huduma ya ‘Stories’ Snapchat ndio ilikua inashika usukani.
Ni wazi mapato na watumaiji wa snapchat walishuka kwa kiasi kikubwa tuu maana wengi waliona hakuna haja sana ya kuingia katika mtandao huo (ambao umeingia) kwani vitu vingi ambavyo vipo katika mtandao bado vipo katika mitandao mingine ambayo watumiaji hao hao walikua wanaitumia tokea zamani.
Ukiachana na yote hayo bado mtandao wa Snapchat haukati tamaa, imekua ikizidi kujiboresha kwa kuongeza vipengele vingi tuu ili kuhakikisha kuwa wanabaki katika ushindani wa kimitandao ya kijamii.
Ni wazi kuwa virusi vya Corona vimeharibu hali ya hewa sana maana kila bishara ambayo ilikua inafanya vizuri haifanyi vizuri tena licha ya kukiwa na zile chache ambazo zimejipatia soko kubwa kupitia janga hili.
Ni wazi kwa huduma kama za kimitandao ya kijamii kukua kwa watumiaji kwa kiasi kwani katika kipindi cha janga hili ni wengi wantumia mitandao ya kijamii kuwasiliana.
Kwa snapchati kupitia robo ya mwaka huu (2020) imekua na taarifa nzuri maana watumiaji wameongezeka katika mtandao huo na pia mapato yameongezeka kwa kiasi kikubwa na hili ni ukilinganisha na robo ya kwanza ya mwaka jana.