Ni wazi kuwa Snapchat ilikuja kwa kishindo kikubwa sana, wengi walikua na matagemeo makubwa sana kuhusiana na mtandao huu. Sio kwamba mtandao haufanyi vizuri, lakini haufanya vizuri sana kama ilivyokuwa matarajio ya wengi.
Kwa sasa wengi wana Snapchat katika simu zao au wana Account za Snapchat lakini hawatumii mara kwa mara mtandao huo, au pengine hawatumii kabisa.
Pengine unaweza ukadhani watu wameamua kuanza kupotezea mtandao huo baada watu maarufu kama Rihanna kukwazana na Snapachat au baada ya mwanamitindo maarufu Kylie Jenner kusema kwamba kwa maoni yake anaona mtandao huo umekufa.
Mtazamo wangu naona kama mtandao huu sana sana unatumika kama uwanja wa kuhariri (ku’edit) picha na video na kisha watumiaji huwa wanachapisha picha/video hizo katika mitandao mingini ya kijamii kama vile WhatsApp, Instagram na Facebook.
Kumbuka inawezekana Snapchat kuwa mtandao namba moja ambao ulikua na ‘Filter’ nyingi na nzuri kuliko mingine ndio maana Facebook na Instagram waliiga hii kitu. Licha ya hivyo picha na video ambazo zina ‘Filter’ za Snapchat bado zinaonekana katika mitandao mingine
Kumbuka kuna watu pia huwa wanatumia tuu kamera ya Snapchat katika kujipiga picha wakidai kamera ya mtandao huu ni nzuri.