Unazifahamu prosesa za simu janja zenye nguvu kuliko zote? Teknokona leo tumekuandalia orodha ya prosesa 5 zenye nguvu kuliko zote pamoja na simu janja zinazotumia prosesa hizo. Kuna makampuni mengi duniani yanayotengeneza prosesa hizi ikiwemo kampuni ya Apple na Samsung.
Prosesa ni kichakataji kinachoiwezesha kompyuta kufanya mahesabu na maagizo mengine ya kimsingi ambayo hupitishwa kutoka kwenye mfumo wa uendeshaji (OS). Uwezo wa kompyuta au simu janja hutegemeana na uwezo wa prosesa kufanya kazi.
Aina 5 za prosesa za simu janja zenye nguvu ni:
Apple A15 Bionic; Prosesa hii hutengenezwa na kampuni ya Apple kwaajili ya simu janja zake na imetumika katika simu janja ya iPhone 13, iPhone 13 Pro, iPhone 13 Pro Max, iPhone 13 Mini na iPad Mini 2021. Prosesa hii ina spidi ya 3.23 GHz.
Apple A14 Bionic; Hii pia ni prosesa iliyotengenezwa na kampuni ya Apple ambayo inatumika katika simu janja ya iPhone 12, iPhone 12 Pro, iPhone 12 Pro Max, iPhone 12 Mini na iPad Air. Prosesa hii ina spidi ya 3.1 GHz.
Snapdragon 888 Plus; Snapdragon ni kampuni kubwa ya kiteknolojia inayojihusisha na utengenezaji wa prosesa za simu janja pamoja na vifaa vingine vya kiteknolojia. Simu janja inayotumia prosesa hii Asus ROG Phone 5S ambayo ni simu janja maalumu kwaajili ya kuchezea magemu. Pia prosesa hii ina spidi ya 3.1GHz.
Snapdragon 888; Prosesa hii ya simu janja ina spidi ya 2.84GHz na simu janja inayotumia prosesa hii ni pamoja na OnePlus 9.
Exynos 2100; Kampuni ya Samsung inajihusisha pia na utengenezaji wa prosesa za simu janja na prosesa hizi huitwa Exynos. Aina hii ya prosesa inatumika katika simu janja ya Samsung Galaxy S21, Samsung Galaxy S21+ na Samsung Galaxy S21 Ultra. Pia prosesa hii ina spidi ya 2.9 GHz.
No Comment! Be the first one.