Asilimia kubwa ya watu huuziwa simu zilizotumika bila ya wao kujua, unaweza kuona simu ipo kwenye box ukafikiri ni mpya lakini uhalisia ni kwamba simu nyingi tunazouziwa huwa zimetumika kisha kurudishwa tena kiwandani au kwenye maduka maalumu ya kampuni husika na kuwekwa kwenye box tayari kwa kuuzwa tena.
Je simu yako imetumika muda kwa muda gani?
Watu wengi hawajui hilo na kujikuta wakiangukia kwenye kununua simu iliyotumika (used), kuna namna mbalimbali za kujua kama simu imetumika kwa mda gani.
- Tumia serial number.
Kampuni nyingi za kutengeneza simu huweza kuweka tarehe ya kutengeneza simu kwenye upande wa Settings >“About phone”, ikiwa imeandikwa kama Hardware information (Taarifa za kifaa) au Manufacturing date (Tarehe ya kutengenezwa), kwa simu za iPhone ukiangalia serial number mfano C38SNP56HFY7 ile namba/digit ya tatu toka mwanzoni ndiyo humanisha mwaka simu imetengenezwa mfano hapo tunaona ni 8 maana yake ni kwamba simu imetengenezwa mwaka 2018 na kama tungeona wameandika C30SNP56HFY7 maana yake simu imetengenezwa mwaka 2010.
2. Tumia Limited Apple warranty.
Kama unatumia simu ya iPhone ukiangalia kwenye “System settings” utaona Apple warranty inaisha lini, yaani warranty huwa ni mwaka mmoja tangu kifaa kianze kutumika kwa siku ya kwanza, kama Apple warranty imeisha mda wake (expire) ujue hicho kifaa kimetumika zaidi ya mwaka mmoja. kama bado haijaisha mda wake itaonyesha inaisha lini.
Kama warranty haipo au huioni kwenye “System settings” unaweza kuiangalia kwenye mtandao (online) kwa kuandika neno “apple coverage” na utaletewa sehemu ya kuandika serial namba ya iPhone na utaona hio apple warranty inaisha mda wake lini (expire date). mfano, iPhone mpya ukiifungua leo inatakiwa ionyeshe muda wake wa kuisha warranty (expire) ni tarehe ya leo ya mwaka unaofata maana yake ni kwamba siku ya leo ndio imeanza kutumika.
Kama utakuta umeandikiwa “coverage expired” ujue hiyo simu imetumika zaidi ya mwaka na imekua refurbished, yaani ilitumika kisha ikarudishwa tena kiwandani kufanyiwa marekebisho na ikapelekwa sokoni tena.
3. Tumia manufacturing codes
Manufacturing codes ni namba yaani “ussd codes” kila kifaa kina manufacturing codes zake kwa ajili ya kutoa/kuonyesha taarifa za hicho kifaa, unaweza kutafuta manufacturing codes za simu yako kwenye mtandao, mfano wa manufacturing codes ni hizi *#*#197328640#*#* au *#197328640#* weka hizo codes kwenye simu baada ya kubonyeza utaenda kwenye sehemu ya “version info” >“hardware version”>“read cal data” na baadae utaona tarehe simu yako imetengenezwa (manufacturing date) ya simu yako na kama simu yako ikikataa hizo manufacturing codes, basi jaribu kutafuta codes zinazoendana na simu yako.
4. kwa watumiaji wa simu za Samsung unaweza kupakua/download programu ya “Phone info app” kwenye Play store ya simu yako na hii ni njia nyepesi sana na itakuletea taarifa zako zote za simu yako mapema sana.
Asante kwa maelezo,ila unakuwa dukani simu inakuwa haijawezeshwa !!
Muuzaji hatakukubalia uweke email kisha ufanye settings ndo upate taarifa hizo. Ukiisha fanya hivyo ukaikuta iliisha tumika,itabidi factory reset?
Ndio, ni muhimu kufanya hivyo kwa usalama wako