Apple wanazidi kuhakikisha kuwa wanatoa vifaa vilivyo bora na vinavyorahisisha maisha ya wateja wao wa kiasi kikubwa sana.
Lakini je, tuko tayari katika kupata huduma ya kamera kwenye saa? kwa sasa kuna saa nyingi tuu ambazo zina huduma hii.
Fikiria kutumia saa tuu yenyewe katika swala zima la kupiga picha moja kwa moja? kuna saa janja nyingi sana zinatumika katika kupiga kamera za simu janja.
Bado jambo hili halipo wazi sana kwani lipo katika hatua za mwanzo mwanzo kabisa, hivyo kwa sasa hakuna taarifa kamili juu ya lini kifaa hiki kitaingia sokoni.
Lakini bado kwa sasa ni jambo gumu kidogo katika kuhakikisha kamera inakaa katika saa hiyo ambayo ni ndogo, na hapo bado hata sijafikiria kuhusiana na flash.
Nadhani majibu yote yatapatikana baada ya kifaa hiki kuingia sokoni sio? kumbuka sio kila kifaa kinachotangazwa na kampuni lazima kiingie sokoni.
Kumbuka Apple watangaza kifaa ambacho kinachaji saa, simu na ipad kwa wakati mmoja, lakini kifaa hicho mpaka sasa hakijaingia sokoni.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa maoni, Hii umeipokeaje na hivi uko tayari kutumia kamera kwenye saa?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.