Apple ni moja kati ya kampuni kubwa inayojihusisha na mambo ya teknolojia, mara kwa mara kampuni hiyo imekua ikileta maboresho au ubunifu wa aina yake ili kujihakikishia inabaki kuwa juu.
Kwa sasa inasemekana kuwa mtandao huo unakuja na huduma ya utafutaji (Search Engine), kumbuka kwa sasa huduma ya utafutaji maarufu ni kutoka katika mtandao wa Google.
Oh, and a new search engine is coming too. Will Siri finally get "smart?" Hmmm.
— Robert Scoble (@Scobleizer) May 28, 2022
Kama hili likiwezekana kumbuka hata Siri itakua imejiboresha kwa kiasi kikubwa kwani itakua inajua vitu vingi sana.
Kwa kiasi kikubwa hapa inamaanisha kuwa SIri itakua imejiboresha katika kujibu maswali, lakini hata hivyo inawezekana huduma hii kutoka Google ikawa inachuana sambamba na huduma zingine kutoka Google (Google Search) na Microsoft (Bing).
Based on a tweet from @Scobleizer (who says it's not a guess, he's heard it from many places…) -> Apple is expected to tease a *new search engine* connected to Siri at WWDC 2022 on 6/8 https://t.co/JUKL6buXhY pic.twitter.com/MW7ueyccoo
— Glenn Gabe (@glenngabe) May 30, 2022
Google imeshalipa mamilioni kwa Apple ili kuhakikisha kuwa inakuwa ni sehemu kuu ya matafuto (Default Search Engine) katika vifaa vya Apple.. SOMA >>HAPA<< na >>HAPA<< kuelewa zaidi kuhusiana na hili.
Haya tukitegemee sasa, kama hili likiwezekana itakua ni moja kati ya machaguo muhimu ya uwekezaji ambayo wamefanya
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Uwanja Wa Comment, Niambie Hili Umelipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.