Matumizi ya rasilimali watu katika kufanya shughuli mbalimbali zikitafutiwa mbadala wake na kwa sasa teknolojia ambayo inayotumiwa kwa nguvu ni ‘Utashi usio halisi‘ ambapo kwa mara ya kwanza ametambulishwa mwandishi wa habari wa kwanza duniani ambae si binadamu.
Katika hali ya kuishangaza duniani hasa waliopo kwenye sekta ya habari (kwa mtazamo wangu) nchini Uchina Nov, 9 2018 waliweka historia ya kumtambulisha mwanahabari ambae kwanza si binadamu, anatumia utashi ambao sio halisi (Artificial Intelligence) na ana uwezo wa kufanya kazi kwa saa 24, siku 365 katika mwaka.
Mwandishi wa habari wa kwanza duniani ambae si binadamu.
Mwanahari huyo ambae ndipo teknolojia inapoelekea kwa sasa na binafsi nikiamini kuwa wanaotafuta/watangazaji habari wanaweza kukosa kazi kwa sababu kuu mbili; uwezo wa kufanya kazi kila leo lakini pia kuweza kuzungumza lugha mbalimbali (zaidi ya moja).
Wakati wa uzinduzi wa wanahabari hao mmojwapo alitangaza kwa Kichina na mwingine akatangaza kwa lugha ya Kiingereza. Pia mwanahabari huyo anaweza kunakiliwa katika matukio tofauti tofauti kuleta habari.
Mwanahabari amabae si bindamu wakato wa utambulisho.
Wakati wa kutangaza habari kwenye shirika moja huko Uchina mwanahabari huyo alijinasibu kuwa ikiwa kitu kipo katika maandishi basi anaweza kutangaza kama mtangazaji.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|