Mgonjwa napoenda hospitalini kwa ajili ya matatizo ya macho daktari wa macho ndio kimbilio lake lakini miaka inakwenda na teknolojia inakuwa, sasa mashine una uwezo wa kubaini magonjwa ya macho.
Kikundi kinachofahamika kama DeepMinds wametengeneza mashine inayotumia “Werevu wa kufikirika” (Artificial Intelligence) na kwa ushirikiano wa madaktari kutoka hospitali ya macho ya Moorfields wamethibitisha kuwa kifaa hicho kina uwezo wa kutambua magonjwa ya macho kwa ufasaha kabisa unafikia 94%.
Hatua inazopitia kifaa hicho ni mbili ambapo inaangalia retina kwenye jicho la mgonjwa kisha baada ya hapo kile ilichokibaini kinapitishwa kwenye mashine tano tofauti kabla ya kutoa majibu kamili.
Kifaa hicho pia kinaweza kutoa kipaombele kulingana na tatizo la mgomjwa na hivyo kufanya mlengwa kupatiwa matibabu kwa haraka hatimae kuondoa uwezekano wa kupoteza uwoni.
Teknolojia hiyo mpya utambuzi wa magojwa ya macho inaelezwa kufanya kazi na kutoa majibu kwa haraka zaidi ukilinganisha na kasi ya madaktari wa macho.
Kwa sasa kifaa hicho bado hakijaanza kutumiwa lakini hatua inayofuata ni kufanyiwa majaribio kwenye hospitali mbalimbali pamoja na kupewa kibali baada ya mamlaka husika nchini Uingereza kukiidhinisha.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|