Kila baada ya muda fulani mfumo endeshi tu bila ridhaa ya yule anaetumia kifaa husika inatunza kumbukumbu za kwenye simu, tabiti, na kuzihifadhi wanapopajua lakini sasa hilo linaenda kubadilika hasa kwenye Android.
Tunapokuwa tumeunganisha vifaa vyetu kwenye intaneti (vinavyotumia Android/iOS) basi tambua tu kwamba kuna wakati mfumo endeshi unaanza tu ktunza vitu kama namba za simu, tarehe muhimu ulizoziainisha kwenye kalenda, n.k kitu ambacho kinachangia katika matumizi ya kifurushi cha intaneti.
Katika maboresho ya hivi karibuni kwenye baadhi ya simu janja mathalani Google Pixel 2 imeonekana Google wameweka kitufe ambacho kinakuruhusu kufanya maamuzi ya kutunza kumbukumbu kwa hiari!.