Mara nyingi tumekutana na hili jambo ambapo watu wanaotuzunguka wanauliza kama kompyuta zao zina uwezo wa kupokea programu endeshaji ya windows 10.
Hii inaweza ikawa mtu anataka kusasisha toleo la mbele zaidi baada ya kuwa anatumia toleo la nyuma (windows XP, windows 7 n.k). Sasa ili kupata toleo kubwa kabisa inabidi kompyuta yako iwe na sifa fulani
Cha msingi kujua hapa ni kwamba kama kompyuta yako tayari ina windows 7, kuna hati hati kubwa kuwa itaruhusu toleo la windows 10 bila tatizo lolote. Kwa kifupi ni kwamba windows 10 na windows 7 zina mahitaji sawa ila kukaa katika kompyuta husika.
Mahitaji Hayo Ni Haya Hapa!
- CPU: 1GHz au zaidi
- RAM: 1GB kwa ajili ya 32-bit Windows au 2GB kwa ajili ya 64-bit Windows (au zaidi)
- Hard Disk: 32GB au zaidi
- Graphics Card: Inayoendana na DirectX 9 au mpya zaidi yenye driver ya WDDM 1.0
Ni wazi kuwa window 10 na 7 zinashabihiana katika swala zima la mahitaji ina kuna utofauti mdogo sana baina ya wawili hao. Windows 10 kwa haraka haraka ni lazima itakuwa inahitaji ujazo mkubwa wa hard disk ukilinganisha na windows 7.
Mpaka hapo nadhani utakua huna maswali mengi juu ya ni windows ya aina gani inaweza ikaingia katika kompyuta yako kwani TeknoKona imekufumbua macho leo.
Chanzo: Microsoft