Machapisho ya kisiasa Facebook yanataanza kuonekana mara chache zaidi kwenye utumiaji wa kawaida wa mtandao huo wa kijamii.
Facebook wamesema wanaanza kufanya majaribio ya teknolojia yao ya kupunguza mara ambazo machapisho/post ya kisiasa yanawafikia watu katika eneo la nyumbani(timeline) la mtandao huo wa kijamii.
Majaribio hayo yanaanza kufanyika nchini Kanada, Brazili na Indonesia, ndani ya wiki chache zijazo jambo hilo hilo litawafikia watumiaji wa Facebook wa nchini Marekani.
Tayari Facebook walishaanza kuwaonesha (recommend) watumiaji wake makundi (groups) ya kujiunga yanayojihusisha na maongezi ya kisiasa.
Suala hili linaonekana kuhusishwa mara moja na kuepuka masuala ya kisiasa kuja kuleta madhara mengi kama iliyovyotokea Marekani ambapo mashabiki na wafuasi wa Rais aliyepita Bwana Donald Trump walishambulia bunge la nchi hiyo ili kupinga ushindi wa Rais Biden. Inasemekana mipango ya maandamano na mashambulizi hayo yalifanyika kupitia mitandao ya kijamii, na kwenye Facebook mipango ilihusisha makundi/groups pamoja na kurasa rasmi/Pages.
Mfumo wa kile unachoona unapoingia Facebook/timeline, inahusisha teknolojia mbalimbali za kutambua vitu unapenda na vile ambavyo huwa nashiriki katika mazungumzo navyo.
Kwa kupunguza masuala ya kisiasa kuja kwenye timeline Facebook wanaamini itapunguza watu kujikuta katika mazungumzo ya kisiasa yasiyo na tija.
Baada ya majaribio Facebook wanategemea kuleta maboresho hayo kwa watumiaji wake wote. Kwa sasa bado hawajasema hii itakuwa lini.
No Comment! Be the first one.