Siku hizi imekuwa sio kitu cha kushangaza kuona kampuni ikiendelea kutoa simu rununu kutoka kwenye familia moja (mtiririko fulani) mpaka hapo watakapoona inafaa kufanya hitimisho. LG wametangaza ujio wa LG V40 ThinQ lakini kiaina.
Kupitia tovuti mbalimbali (tukiwemo na tssisi wenyewe, teknokona) wamekuwa na shauku na kutaka kujua simu janja LG V40 ThinQ itakuwa na vitu na sifa gani lakini juhudi hizo zimegonga mwamba ingawa taarifa rasmi kutoka kwa LG ambao wamebainisha vitu vichache tuu ambavyo vipo kwenye bidhaa husika:
Kioo/Rangi.
Katika hali ya kudokeza LG wamebainisha kuwa simu hiyo kioo chake kitakuwa na urefu wa inchi 6.4 pamoja na rangi mpya; kulingana kwa Kishwahili tulichokizoea ni “Damu ya mzee”.
Kamera.
Katika vitu ambavyo vilionekana wazi ni idadi ya kamera ambazo zipo kwenye LG V40 ThinQ ikionekana dhahiri kuwa ina jumla ya kamera tano (5); kamera 3 upande wa nyuma na mbili kwa mbele.
Hakuna kitu kingine ambacho kimeshabainika kuhusu simu hiyo ila kila kitu kitajulikana Okt. 3 2018 ambapo ndipo itakapozinduliwa rasmi.
Vyanzo: Engadget, GSMArena