iPhone 13 kutoka Apple inatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwaka huu, ikiwa ni bado utambulisho wake bado kumekuwa na fununu mbali mbali kuhusiana na vipengele vya simu hiyo.
Moja kati ya hivyo ni ujazo uhifadhi ndani ya simu hiyo…….. kuna vyanzo vinasema simu hiyo itafikia hadi ujazo uhifadhi wa terabaiti moja.
Kama ikitokea hivi hii ndio itakua mara ya kwanza kwa kampuni ya Apple kutoa iPhone ambazo zina ujazo uhifadhi mkubwa kiasi hicho, lakini hata hivyo bado vyanzo vingine vinapinga fununu hizi.
Kitu ambacho kipo wazi ni kwamba simu hiyo itakuja katika hali ya kwamba itakua ni bora zaidi kulinganisha na iPhone 12 na kingine ni kwamba itakuja katika matoleo ya iPhone 13, iPhone 13 mini, iPhone 13 Pro, na iPhone 13 Pro Max.
Licha ya yote uwezo tuu wa ujazo uhifadhi wa TB1 kwa simu janja yoyote ni jambo la kuvutia sana kwai kwa teknolojia jinis ilivyo sasa ni jambo la muhimu sana
Kumbuka sasa kuna uwezo wa 5G duniani hii inafanya kasi ya kushusha na kutumia internet kwa uharaka zaidi hali ambayo inafanya simu kula nafasi nyingi zaidi.. fikiria ukiwa na TB1 katika simu yako sasa..
Sawa ujazo mkubwa wote huo unaweza ukawa sio chaguo la kila mtu lakini kuna wale ambao hili linaweza likawa ndio kimbilio lao mara moja.
Tujiwekee tuu akilini kwamba ujazo wa iPhone 13 unaweza ukawa au usiwe wa 128GB, 256GB, 512GB au 1TB.
No Comment! Be the first one.