Hii ni habari ya kusikitisha hasa kwa wana teknolojia wengi maana bwana John McAfee ni moja katika ya watu muhimu sana katika teknolojia.
Bwana huyu anasifika kwa uvumbuzi wa Anti Virus maarufu sana inayojulikana kama McAfee Anti Virus ambayo aliianzisha mwaka 1987 na amefariki akiwa na miaka 75.
Ifahamike kuwa bwana huyu amefia gerezani huku nchini hispania na sababu za kifo vyanzo mbalimbali vinasema ni za yeye mwenyewe kujitoa uhai wake.
Hili limetokea mara baada ya mahakama ya huko nchi Uhispania kuruhusu bwana McAfee kuweza kuhamishiwa kesi yake na kuhukumiwa nchini Marekani.
Kesi iliyokua inamkabili bwana McAfee ni uhujumu uchumi kwa kutolipa kodi stahiki kwa kuficha baashi ya mali zake na kuficha hela kwa kutumia mfumo wa sarafu za kidijitali.
The US believes I have hidden crypto. I wish I did but it has dissolved through the many hands of Team McAfee (your belief is not required), and my remaining assets are all seized. My friends evaporated through fear of association.
I have nothing.
Yet, I regret nothing.
— John McAfee (@officialmcafee) June 16, 2021
Uhakika juu ya chanzo cha kifo bado haujawekwa wazi (fahamika) kwani serekali ya Uhispania inasema bado inafanya uchunguzi juu ya jambo hilo.
No Comment! Be the first one.