Kwa zaidi ya miaka miwili sasa dunia nzima imekuwa ikipambana na janja la Virusi vya Corona ambalo limeendelea kuchukua maisha ya watu siku hadi siku. Halikadhalika, wanasayansi hawajalala, wanafanya tafiti mbalimbali kubaini njia bora ya kukabiliana nao na pengine kuvitokomeza kabisa.
Mpaka sasa tumefikia awamu ya nne ya kirusi cha Korona kiitwacho Omicron ambacho kiligunduliwa na wanasayansi wa nchini Afrika Kusini lakini na si kwamba vile vingine havipo tena, la hasha! Sasa kuna njia mpya ya kukabiliana na virusi vya Korona ambayo wanasayansi wamegundua ambayo ni “Kiburudisho cha mdomo”.
Wengi wetu huwa tunatafuna kiburudisho hiki cha mdomo ambapo kwa Kiingereza tunasema “Chewing gum” ambapo kwa mujibu wa wanasayansi wamebaini kuwa maambukizi ya virusi vya Korona yanaweza kupunguzwa na kitu hiki. Ipo hivi:
Iwapo mtu mwenye virusi vya Korona atatafuna kiburudisho cha mdomo basi hapa hatakuwa anaondoa tuu uchovu mwilini mwake bali anatakuwa anapunguza virusi vya Corona vilivyopo kwenye mate yake. Kiburudisho cha mdomo kina protini za ACE2 ambacho ndio kitu (protini) kinachotumiwa na virusi vya Corona kuathiri seli.
Nini mantiki yake?
Kugundulika kwa njia hii ya kutumia kiiburudisho cha mdomo kupunguza maambukizi ya virusi vya Korona inamaanisha kuwa iwapo mtu ataongea, kukohoa au kupumua basi kile ambacho kinakuwa kinatoka kwenye mdomo (hewa iliyochanganyika na kiburudisho cha mdomo) inapunguza kwa kiasi kikubwa kutoka kwa aliye na virusi kwenda kwa mwingine.
Haya sasa wapenzi wa kutafuna kiburudisho cha mdomoni kazi kwetu kutumia silaha hii muhimu kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Korona.
Vyanzo: Gadgets 360, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.