Naaam, usishangae umesoma sawa sawa tuu hapo juu, moja ya vipengele ambavyo iOS 16 ilitarajiwa kuja navyo ni uwezo wa mtu kuona asilimia ya chaji isliyosalia katika betri!
Na tuliandika habari hiyo kwa ukubwa kabisa katika chapisho >>HILI HAPA<<

Mambo yamebadilika bwana, tulitegemea kila iPhone ambayo itakua na uwezo wa kutumia iOS hii basi itakua na uwezo wa kuonesha asilimia hiyo ya chaji katika betri, lakini jambo zima halipo hivyo.
Iphone Ambazo Hazitakua Na Uwezo Huo Ni:
iPhone XR
iPhone 11
iPhone 12 Mini
iPhone 13 Mini
Najua hapa utakua na maswali juu ya matoleo ya chini ya hapo na utakua unajiuliza vipi kuhusu iPhone 8 maana tangazo linasema kuanzia 8 kwenda juu wote watapata iOS 16.

Hapa cha kufahamu ni kwamba kipengele hicho hakitakua kwa simu zote kama tulivyotemea hapo mwanzo.
Kwa simu zote tajwa hapo juu kama kupitia iOS 16 hazitakua na uwezo huo basi hakuna budi itabidi watumiaji waingie katika eneo la ‘Control center’ kama wakitaka kuona silimia salia za chaji.
Ikumbukwe hapo awali simu zote za iPhone zilikua zikionyesha sehemu ya eneo la chaja katika simu zote pembeni ya betri.

Baada ya kutoka iPhone X na kuendelea mambo yakaanza kubadilika taratibu na sababu kuu ikiwa Apple walijibakizia uwanja mdogo sana sababu ya ‘Notch’ katika iPhone.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, niambie hii umeipokeaje? Je ni kipengele kikubwa kiasi kwamba hakikutakiwa kuachwa katika baadhi ya iPhone?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.