Xiaomi mwaka huu wameamua kuja na toleo jipya la simu janja ambalo limewekwa vifaa vyenye nguvu maradufu ili kuwezesha rununu husika kufanya kazi kwa ufanisi bila kusahau uchezaji wa magemu kwa kutumia kifaa hichohicho.
Toleo hili la Pro lilitoka sambamba na Xiaomi Black Shark 4 ambazo kwa kuangalia undani wa simu janja hizi utagundua kuwa zimetofautiana sehemu ndogo sana na hivyo kufanya moja kuwa na uwezo zaidi kuliko nyingine.
Kitu cha pili cha kuzingatia ni kwamba Black Shark 4 Pro imetolewa ikilenga soko la Uchina tu jambo linaloifanya simu hii kutopatikana katika masoko mengine. Sasa tupate kuzifahamu sifa za rununu hii kama ifuatavyo:-
Kioo :
- Ukubwa: Urefu wa inchi 6.67
- Ubora: Super AMOLED (1080*2400px, 144Hz); ina ung’avu wa hali ya juu sana kufanya kinachoonekana kivutie
Memori :
- Diski uhifadhi: 256GB/512GB
- RAM: GB 8/12/16
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 64, 8 na 5+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 4K na 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 20+uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4500 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 120W (50% ndani ya dakika 5, 100% ndani ya dakika 15 tu)
Kipuri mama :
- Snapdragon 888 5G
Uzito :
- Gramu 220
Programu Endeshi
- Joy UI 12.5, Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi, Fedha na Bluu
- GB 8/256-$940 (zaidi ya Tsh. 2,162,000), GB 12/256-$825 (zaidi ya Tsh. 1,897,500) na GB 16/512-$995 (zaidi ya Tsh. 2,288,500) bei ya Uchina
Hakika hii ni simu yenye nguvu na inamfaa yeyote yule ambae anapenda kutumia simu janja kufanya vitu vizito iwe kwa ajili ya kuburudika, kuelimika, n.k. Kilichobaki ni wewe msomaji wetu kuchagua mbivu ama mbichi.
Vyanzo: GizMoChina, GSMArena
No Comment! Be the first one.