Wakati kuna simu janja nyingi tuu duniani zikiwa bado hazijapelekwa toleo la Android 12 ili waweze kupakua tayari Google yapeleka inachokitengeneza yaani imeshaanza mchakato wa kufanya programu endeshi inayofuata baada ya hii ya sasa inapitiwa na waundaji mbalimbali.
Leo, Aprili 10 Google imepeleka toleo la kwanza kabisa na la awali la Android 13 kwa waundaji (watalamu wenye uwezo wa kuandika programu na ikafanya kitu fulani) ili waweze kufahamu kile ambacho wamepanga kuleta kwa watu wanaotumia rununu zinazoendeshwa na programu endeshi.
Katika kile ambacho kimeonekana kwenye Android 13 (toleo la awali) ambalo kimsingi linapatikana kwa watu wachache sana na kimsingi uandishi wa programu endeshi bado upo kwenye hatua za awali kabisa imeonekana Google wanapanga kuboresha maeneo mbalimbali mathalani kuumpa mtu wezo wa kusambaza kitu kwa wengine bila ya kuombwa kuruhusu mfumo uweze kuinigia ndani kuangalia kilichopo.
Kitu kingine ambacho kitakuwepo kwenye Android 13 ni uwezo wa mtu kuunganisha na intaneti isiyotumia waya (WiFi) iliyopo karibu bila ya kuombwa ruhusa ya kutaka kujua mahali wewe ulipo. Halkadhalika, mtu atakuwa na uwezo wa kuandika vichwa vya habari kwenye vile vitu ambavyo atapenda kuvipangalia kwa haraka (kuvifikia kwa wepesi).
Google yapeleka Android 13 kwa waundaji lakini je, itatoka lini?
Google wameipeleka Android 13 kwa watalamu lakini kwa namna moja au nyingine inaonekana kutakuwepo mahusiano ya karibu kabisa ili kufanya wanakuja na programu endeshi ya tofauti na bors kuliko hii ya sasa. Hapa katikati Google itakuwa ikitoa toleo la majaribio ambalo kila baada ya muda fulani lakini Android 13 yenyewe kabisa inatazamiwa kuja mwezi Julai.
Kama mtu ni mtalamu wa kuandika programu na angependa kuwa miongoni mwa wale wanaopata vionjo vya kwenye Android 13 basi BOFYA HAPA kuweza kupakua toleo hilo mahususi kwa ajili ya waundaji lakini lijaribiwe kwenye simu janja za Pixel 4 kwenda juu.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.