Katika kusaidia bidhaa za mbalimbali za Apple kuweza kupatikana kirahisi mara zinapopotea AirTags kimekuwa ni kifaa muhimu sana kwa wale ambao wanapenda kuweka ulinzi kwenye vitu vyao vya kidijiti.
AirTag kifaa kidogo (mithiri sarafu) ambacho kinatengenzwa na Apple kazi yake ikiwa ni kumuwezesha mtu kupata kifaa chake ambacho anakifuatilia mahali kilipo; yaani mfano una iPhone 12 Pro halafu unataka ikipotea iwe rahisi kidogo kuifuatilia na kufahamu mahali ilipo basi unabandika AirTag kisha unaiunganisha kwenye simu/saa janja ili kuweza wapi kilipo kila wakati.
AirTag imeonekana kuwa shubiri kwa wengine ambapo watumiaji wanaitumia kuwafuatilia watu wengine mathalani wapenzi bila yao wao kujua kitu ambacho ni kosa kisheria. Sasa Apple wanajipanga kuleta maboresho ambayo yatafanya watu kuweza kujua wana AirTag ambayo si ya kwake.
Kwa kuanza Apple itaboresha kwa kuweka angalizo kwenye hatua za mwanzo kabisa wakati wa kuunganisha mawasiliano ya AirTag kwamba ni kosa kisheria kumfutatilia mtu bila idhini yake. Vilevile, Apple inapanga kupeleka maboresho kwenye AirPod Pro, AirPod Max na kizazi cha tatu cha AirPod halikadhalika vifaa vingine ambavyo vinaweza kuuanganisha AirTags ambapo mtu hatapata taarifa kwenye simu janja kuwa kuna kitu kisichojulikana kimebainika na badala yake programu endeshi (iOS) itamwambia wazi kuwa unasafiri na AirPods za mtu mwingine ili kuondoa mkanganyiko.
Baadae mwaka huu Apple pia itapeleka maboresho kwenye iPhone 11, 12 na 13 kuwawezesha watumiaji wake kwenda kupata AirTag zao ambazo kwa mwingine si chake hivyo kufanya kurejea kwa mwenye mali yake.
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.