Teknolojia inakuwa na lengo kuu likiwa ni kurahisisha mambo ili yaweze kwenda vizuri, programu kama VLC Player na AirPlay sio vitu vigeni kwa watu wanafuatilia teknolojia.
AirPlay ni nini?
AirPlay ni mkusaniko wa programu ambao unaruhusu mawasiliano kwa kutumia teknolojia isiyotumia waya kuona, kusikiliza au kutuma vitu kutoka kifaa kimoja hadi kingine.
Sasa watumiaji wa vifaa vya Apple/Android watafurahi kutokana na kie ambacho kinaonekana kuwa kitawavutia wengi hasa kwa sababu VLC player imeshashushwa mara bilioni 3. Hii ni kwa sababu VLC watarajiwa kutoa sasisho ambalo litaruhusu mawasiliano kuka kwenye kifaa cha Apple/Android kwenda kwenye Apple TV.
Kwa lugha rahisi ni kwamba mtu mwenye bidhaa ya Apple/Android ataweza kutuma miziki, picha jongefu kutoka kwenye vifaa vyao kwenda kwenye Apple TV.
Kujuisha kwa programu ya AirPlay kunatazamiwa kuja hivi karibuni kwani hakuna tarehe rasmi iliyotangazwa kuwa sasisho hilo litatoka. Je, wewe umepemdezwa na kitu hicho kipya kitakachokuja katika siku za usoni?
Vyanzo: The Verge, 9to5Google