Google Pixel ni simu janja nzuri sana na zinasifika sana katika katika swala zima la picha na hata utendaji wake wa kazi.
Google kupitia simu yao mpya inayokwenda kwa jina la Google Pixel 6A, ambayo wameitangaza hivi karibuni, inakuja na vipengele vingi lakini sio tundu la spika za masikio.
Hii kwa maana nyingine Google kupitia simu hiyo wanajiunga katika chama cha simu zingine ambazo zilaiachana kabisa na tundu hilo mfano mzuri ni simu za iPhone.
Lakini hii haimaanishi kwamba matoleo mengine ya Pixel yatakuwa hayana tundu hilo, lakini pia haimaanishi kama hayatakua nalo —umeelewa hahaha?
Kumbuka pia kampuni ya Google ina spika za masikio ambazo hazina nyaya (Wireless) pengine ndio watakua wanatumia kigezo hiki ili kuweza kuuza bidhaa hiyo.
Kwa sasa matoleo ya simu ya Pixel kutoka Google yanafanya vizuri sana katika soko, tuone na toleo hili litafanya vipi katika soko.
Niandikie hapo chini katika uwanja wa comment maono yako ni yapi katika swala hili zima la kutoa tundu la spika za masikio katika simu janja?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.