Fununu zinasema mpaka kufikia 2023 kwa iPhone ambazo zinakuja basi zitakua na sehemu ya kuchaji ambayo tundu lake litakua ni lile la Type-C.
Kumbuka aina hizi za chaja simu nyingi za Android ndio zinatumia. Kumbuka habari nyingi kuhusiana na iPhone na charger ya ina hii vimehusishwa sana
(1/2)
My latest survey indicates that 2H23 new iPhone will abandon Lightning port and switch to USB-C port. USB-C could improve iPhone's transfer and charging speed in hardware designs, but the final spec details still depend on iOS support.— 郭明錤 (Ming-Chi Kuo) (@mingchikuo) May 11, 2022
Wengi wakisema ni jambo zuri na wengine wakidai kuwa sio jambo jema kuanza kuaingiliana charge na makampuni mengine ya simu.
Kumbuka asilimia kubwa sana ya soko la simu janja wote wanatumia au wameikubali teknolojia ya USB-C (Type-C) katika chaja zake.
Kuna kipindi Apple ilikua inapinga vikali chaja za aina nyingine ukiacha na chaja zao, wengine wanasema kuna muda walitaka kuchukua maamuzi magumu zaidi.
Maamuzi yenyewe ni kwamba walikua wako radhi katoa tundu la chaja kabisa na kuanza kutegemea chaja zao zile za bila nyaya.
Hakuna mambo mengi sana kuhusiana na jambo hili, lakini kama kawaida yetu tukipata za kina kabisa tutakuletea hapa hapa katika mtandao wako pendwa.
Niandikie hapo chini katika eneo la comment, hii umepokeaje? napenda kusikia kutoka kwako sana wewe ambae ni mtumiaji wa iPhone…
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.