Sony Xperia Ace 2 ni simu janja ambayo kwa wiki kadhaa imekuwa ikitolewa sifa zake ingawa hazikuwa rasmi lakini hilo sasa linakaa kando kwani rununu hiyo imezinduliwa leo huko Japan.
Sony imeendelea kuangalia aina mbalimbali za wateja kwa maana ya kwamba wale ambao wanaoweza kununua simu janja zenye uwezo wa juu sana na upande wa pili kuna wateja wanaonunua rununu zisizo na mengi. Ndio, Sony Xperia Ace 2 inaangukia kwenye kundi la simu ambazo zina sifa za kawaida kama zinavyosomeka hapo chini:
Kioo :
- Ukubwa: inchi 5.5
- Ubora: IPS LCD HD+; ina ung’avu wa hali ya juu sana kufanya kinachoonekana kivutie+ Kioo chake ni Gorilla Glass 6 kwa uso wa mbele
Memori :
- Diski uhifadhi: GB 64+uwezo wa kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 4
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 13 na MP 2+taa ya kuongeza mwangaza sehemu hafifu
- Kamera ya Mbele: MP 8
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4500 mAh
- USB 2.0
Kipuri mama :
- Helio P35
Uzito :
- Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi, Nyeupe na Bluu
- GB 4/64-$202 (zaidi ya Tsh. 464,600) bei ya Japan
Ingawa tayari imeshazinduliwa lakini simu hii itaingia sokoni Mei 28 ya mwaka huu. TeknoKona inamini simu hii itapata wateja wengi kutokana na sababu nyingi lakini kuwa zaidi bei yake inahimilika.
Vyanzo: GSMArena, Mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.