Siku baada ya siku teknolojia inazidi kukua na kuleta mambo mapya lakini pia hata kuboresha vile ambavyo vipo na vinatumiwa. Masuala ya mahesabu ni muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku na sasa mambo yamerahisishwa kwenye hilo kwa kutumia nguvu ya teknolojia.
Katika ulimwengu wa teknolojia ya leo unaweza usitoke na nyaraka yoyote mkononi na kwenda nayo pahali pa kazi na bado ukaweza kufanya shughuli zako vizuri tuu. Hapa siri ni kwamba umehifadhi vitu vyako huko kusikojulikana na una uwezo wa kuvipata wakati wowote, mahali popote.
Mbali na hilo naamini kuna wale ambao wanapata changamoto ya kufanya hesabu fulani fulani hivyo kusababisha kukosea na hivyo kutoa jibu lisilo sahihi. Kwa wale wana mahesabu na wamesahawahi kuandaa nyaraka mtandaoni inahusisha kupiga hesabu naamini wanaifahamu Google Sheet ambayo ni sawa na Microsoft Excel.
Katika maboresho ambayo yamefanyika kwenye Google Sheet hivi sasa kisaidizi hicho sasa kinaweza kupiga hesabu fulani fulani na kutoa jibu kulingana na data ulizoziandika. Kutokana na ukuaji wa teknolojia mathalani hivi sasa ukiweka alama ya sawasawa (=) mara mwisho wa data uliziingiza basi mashine itatafuta jumla, wastani wa kile ulichokiandika.
Mbinu inayotumika hapa mashine inaangalia hata vichwa vya habari ili kuweza kutoa pendekezo ya kile ambacho kinahitajika kufanyika mwisho wa kuandaa nyaraka husika.
Lakini mambo ni mazuri kwa mapana yake kwani kote kwenye Excel, Google Sheet kuna data ukiziandika mwanzo wake tu mashine ikamaliza mpaka mwisho wake. Mfano ukiandika namba kwa kuruka moja moja au mbili mbili, ukaandika siku chache za wiki na yenyewe ikamalizia baada ya kuiamuru.
Maboresho hayo kwenye Google Sheet yameanzia kwa wanaotumia Workspace, G Suite na akaunti binafsi za Google na pengine ndani ya siku 15 zijazo watu wote wataweza kuona kitu hicho kipya ambacho kinarahisisha kupiga hesabu 😀 😀 .
Mwisho wa siku usiamini sana mashine kwa asilimia zote hivyo daima kumbuka kukagua majibu hasa pale ambapo uiamuru itafute majibu kwa kuchukua data nyingi kwa wakati mmoja.
Vyanzo: The Verge, Gadgets 360
No Comment! Be the first one.