Sakata la simu za Samsung Note 7 kulipuka kwa watumiaji wengi duniani kote lilikuwa moja kati ya sakata kubwa zaidi kulikumba kampuni la simu katika miaka ya hivi karibuni. Baada ya kuchunguza kwa muda mrefu Samsung imesema kuwa betri za simu hiyo ndiyo zilikuwa na mushkeli!
Uchunguzi uliofanywa na Samsung kuhusu visa vya simu aina ya Galaxy Note 7 kushika moto, umebaini kwamba suala hilo lilitokana na kasoro kwenye ubunifu na utengenezaji wa mabetri ya kutumika kwenye simu hiyo.
Kampuni hiyo iliacha kutengeneza na kuuza simu hizo Oktoba mwaka jana baada ya visa hivyo kuripotiwa kwa wingi. Simu ambazo zilitolewa upya pia zilikuwa zinashika moto.
Taarifa kutoka Samsung zinasema kuwa tatizo la simu hizo halikutokana na programu za simu hiyo iliyotarajiwa kutoa ushindani kwa simu za iPhone zinazotengenezwa na kampuni ya Apple.
Ushindani wa kiubunifu katika kutengeneza simu janja nyembamba zaidi na yenye kukaa na chaji kwa muda mrefu zaidi unaonekana kuleta changamoto kubwa katika kuhakikisha usalama unazingatiwa katika ubunifu na utengenezaji wa mabetri kwa ajili ya simu hizo.
Kampuni hiyo imesema kasoro kwenye uchoraji wa muundo wa betri hizo pamoja na kasoro kwenye mfumo wa utengenezaji wa betri hizo, zilisababisha betri hizo ambazo ziliundwa na kampuni mbili kuwa na kasoro.
Samsung imesema inawajibika kutokana nabetri hizo kuwa na kasoro na kuthibitisha matatizo yaliyotokana na muundo wa betri na kasoro kwenye uundaji wa betri.
Kumbuka kusambaza makala na pia kuungana nasi kupitia Facebook, Twitter, Instagram, YouTube, Telegram na Google Plus
Chanzo: BBC
2 Comments
Comments are closed.