Kutokana taarifa iliyochapishwa na mtandao wa bloombergy inasema kuwa kampuni ya Apple ipo katika matengenezo ya iPad Pro mpya ambayo itakuwa na uwezo wa kuingiza chaji bili waya.
Kwa kiaisi kikubwa teknolojia hii sio jambo la kushtua (kwa kipindi hiki) maana hata katika iPhone kuna baadhi ya matoleo ambayo yanatumia teknolojia hii.
Vile vile bloombergy wamesema katika ripoti yao kwamba ili kampuni kuendana na teknolijia hiyo ya ‘wireless charging’ katika tabiti hiyo inayokuja basi inabidi tabiti hiyo iwe na umbo lake la nyuma liwe la kioo
Pia hili sio la ajabu sana kwani tuliliona kupitia iPhone 12 ambapo umbo lake la kii linakuwa kama ni njia ya kuunganisha na MagSafe ambayo ndio huwa inasaidia simu hizo ziweze kuingiza chaji.
Kuhusiana na sifa za undani za tabiti hii bado hazijawekwa wazi, lakini pindi tukizipata utakuwa wa kwanza kuzijua.
No Comment! Be the first one.