Kwa miaka kadhaa sasa Google imekuwa ikimlipa Apple mabilioni ya dola kwa sababu za kibiashara hususani ndani ya kivinjari cha Safari; kwa mwaka huu mambo ni hivyo hivyo tuu.
Makubaliano ya Google na Apple kuhusu wao (Google) kuwa ndio wanaonekana kwenye uso wa mbele iwapo mtu atataka kutafuta kitu mtandaoni ndani ya kivinjari cha Safari yanarudi mwaka 2005 ambapo mwaka 2007 iPhone ilipotoka, mkataba wao uliendelea na Apple walilipwa $3 bilioni mwaka huo.
Mwaka 2021, Google imeamua kutoa tena mabilioni ya dola kwa Apple ambapo kiasi cha $15 bilioni kimeshalipwa kwa Apple ili kuendelea kuwafanya Google ndio ndio wanaonekana kwanza bila kumpa mtumiaji wa kuperuzi kwingineko kama Bing ambayo inamilikiwa na Microsoft.
Gharama za makubaliano hayo zimekuwa zikiongezeka mwaka hadi mwaka ambapo mwaka katika miaka ya karibuni mathalani 2020 Apple ililipwa na Google $10 bilioni, $8 bilioni (2019).
Je, kwanini Google inatumia pesa nyingi kumlipa Apple kila mwaka?
Jibu la swali hili ni mbinu tuu ya kibiashara kwa kutaka kuwa chaguo la kwanza kwa wote wanaotumia iPhone, iPad, Macbook, n.k hasa akiwa analenga kuwa mbele zaidi ya Microsoft kupitia Bing ambapo inaonekana kuwa ndio chaguo la pili baada ya Google ndani ya kivinjari cha Safari.
Wachambuzi wa masuala ya fedha wanasema kuna uwezekano wa Google kuilipa Apple kati ya Bilioni $18 hadi $20 mwaka unaokuja ili kuendelea kuwa chaguo la kwanza kwenye kivinjari cha Safari.
Vyanzo: Gadgets 360, Gizmodo
One Comment