Inawezekana kabisa wewe ukawa ni mmoja kati ya watu wengi duniani ambaao wanacheza gemu/magemu kama sehemu ya kujiburudisha, kuingiza kipato, n.k kupitia simu janja, kompyuta au kifaa kingine.
Kwa baadhi ya watu kucheza gemu imekuwa ni sehemu ya maisha yao na si ajabu tukawa tunalifahamu gemu la “Farm Ville” ambapo limekuwepo kwa muda wa zaidi ya miaka 11 lakini itakapofika Desemba 31 kiburudisho hicho hakitaweza kupatikana tena. Sababu ya uamuzi huo ni kuonekana kuwa sio tena kipenzi cha mamilioni ya watu duniani kote.
Gemu hilo ambalo limekuwa likichezwa sana kwenye Facebook linawezesha watu kushirikiana kwa pamoja kwenye kilimo na kwa mujibu wa muundaji wake, Zynga wakati umefika wa kuachana na kiburudisho hicho kilichowaleta watu wengi pamoja mtandaoni.
Mwaka 2009, gemu hili lilikuwa na watumiaji zaidi ya milioni 10 kwa siku na takwimu za juu zinaonyesha kuwahi kufika karibu milioni 30 katika kipindi cha miezi miwili.
Tayari Adobe wanajipanga kuacha kutoa masasisho ya Flash Player ikiwa kama kiungo muhimu cha kuwezesha Farm Ville kuchezeka kupitia kwenye wavuti (Facebook) na Nov. 17 huduma ya kuweza kulilipia itasitishwa ingawa litaendelea kupatikana hadi Desemba 31.
Vyanzo: Engadget, The Verge
No Comment! Be the first one.