Kila sekunde watu wanafikiria kitu kipya cha kufanya ama kuleta kwenye ulimwengu wa teknolojia na hakika tumeshaona/kusikia mengi tuu ila kazi baddo inaendelea. Je, umesikia kuhusu uwezo wa kufanya malipo kwa kutumia kiganja?
Teknolojia imeleta vitu vingi ambavyo vinahakikisha usalama wa mtu au kitu fulani; tunafahamu kuhusu kutumia msimbo, alama za vidole, mboni ya jicho yote hii ni kufanya mahali husika pawe na usalama wa aina yake na pengine wa hali ya juu. Sasa unaweza ukashangaa kusikia kuhusu uwezo wa kufanya malipo kwa kutumia kiganja cha mkono.
Huko Seattle-Marekani kwenye maduka mawili ya Amazon-Go ambayo kuna huduma inayoruhusu mtu kuweza kuingia kwenye duka, kufanya malipo bila ya kuwepo mawasiliano ya ana kwa ana kati ya mtunza pesa na mteja; mtu anaingia kuchagua anachotaka kununua kisha kuruhusu malipo kwa kutumia kiganja cha mkono.
Kupitia mashine maalum inachomekwa kadi ya benki ambapo ambapo baada ya sekunde chache baada ya taarifa za mhusika kulandana na kiganja chake cha mkono basi ataweza kuruhuswa kuingia dukani (iwapo ni mara yake ya kwanza) au kuwezesha malipo kufanyika.
Teknolojia hii inaweza kuwa nzuri kwenye maeneo mbalimbali ambayo yanaleta mkusanyiko mkubwa wa watu mathalani vituo vya mabasi, gari moshi, viwanja vya ndege, maduka makubwa, n.k. Waswahili wanasema “Tembea uone” lakini sisi tunakuletea habari kuhusu teknolojia hapohapo ulipo. Usiache kutufuatilia kila leo.
Vyanzo: Engadget, The Verge
No Comment! Be the first one.