Samsung hivi sasa wanafahamika kwa simu yao ya kujikunja (Galaxy F) ikiwa na sifa lukuki ambazo zinatokana na ukuaji wa teknolojia. Galaxy F inafahamika kuwa simu ghali zaidi ambazo Samsung wameshawahi kutoa na sasa hata bei ya mifuko kwa ajili ya bidhaa hiyo imeshafamika.
Ili simu iweze kudumu mbali na kubebwa na utunzaji wa mtu husika lakini mfuko (case) ambao unatumika kuivalisha simu husika pia inachangia kwa kiasi kikubwa rununu husika kuweza kudumu/kutodhurika kirahisi kutokana na mambo mbalimbali.
Kwa wale ambao tunakusanya nguvu kuweza kununua Samsung Galaxy Fold mara zitakapoingia sokoni ni vyema tukafikiria kutenga kiasi cha fedha kuweza kununua mfuko mahususi kwa simu hiyo ambapo bihaa hiyo (mfuko) itauzwa kwa $119|zaidi ya Tsh. 273,700 kwa bei ya ughaibuni. Kuhusu rangi za mifuko hiyo mpaka sasa ni mbili tu ndio ambazo zimeweza kufahamika; Nyeusi na Nyeupe lakini huenda yakaja katika rangi tofauti tofauti mbali na ambazo zimekwishafahamika.
Ukiamua kuwa na simu nzuri na iliyo kwenye vinywa vya watu kwa maana ya kuzunugmziwa kwa sana basi huna budi kuandaa pesa nyingi tuu kuweza kununua Galaxy F yenye pamoja na mfuo wake kuifanya rununu kuwa salama zaidi kuliko kubaki ikiwa tupu.
Vyanzo: GSMArena, iGywaan Network