Sasa ni muda wa kusema kwaheri iTunes. iTunes ni moja ya app maharufu kutoka Apple kwa ajili ya kompyuta za Windows na Macs. Ni app ambayo iliwaletea mafanikio makubwa kibiashara.
Baada ya miaka mingi ya kuendelea kutumika bila mabadiliko makubwa ya utendaji wake sasa Apple wametangaza rasmi ya kwamba muda wa app hiyo kufanyiwa mabadiliko umefika – na haitakuwa mabadiliko tuu bali ni kuondolewa kabisa kwa app hiyo maarufu.
Uondokaji wake unaleta app 3 za kujitegemea. Kutakuwa na programu ya Apple Music, Apple TV na app mpya ya Podcast (Je unataka kujifunza Podcast ni nini? – Soma hapa Teknokona/Podcast)
Mabadiliko haya yatakuja rasmi kwenye sasisho jipya la programu endeshaji ya Mac OS inayokwenda kwa jina la Catalina ambayo ipo katika hatua za mwisho wa utengenezaji. Tunategemea baada ya hapo matoleo kwa ajili ya kompyuta za Windows yatafuata.
Kwa MacOS watu wataweza kufanya uhifadhi wa data (backup) wa simu za iPhone moja kwa moja kwenye programu ya mafaili ya Finder – kazi ambayo zamani ilikuwa inafanyika kwenye iTunes.