Kampuni ya mawasiliano ya Halotel imezindua kifurushi kipya kisichoisha kitakachowawezesha wateja wake kufanya mawasiliano bila kikomo.
Kifurushi hicho kinakachofahamika kama ‘SuperHalo‘ wateja wa Halotel watakaojiunga na kifurushi ambacho watapiga simu au kutumia intaneti hadi kitakapokwisha bila kujali muda wa kujiunga.
Mkuu wa kitengo cha mawasiliano kwa umma wa kampuni hiyo, Mhina Semwenda amesema kifurushi hicho kinaondoa ukomo wa muda wa vifurushi vya maongezi na intaneti.
Kifurushi cha SuperHalo kinawezesha wateja wa Halotel kupata mawasiliano bila ya wasiwasi wa kuisha muda wa matumizi hivyo kukidhi mahitaji yao ya kiuchumi na kijamii. Wateja wa Halotel wanaweza kujiunga kuanzia Tsh. 500 kupata kifurushi cha Super Halo kwa kupiga namba *148*66# kisha utachagua SuperHalo.
Utaratibu uliopo sasa kwenye kampuni nyingi za simu ni kuwa na vifurushi vyenye ukomo kwa mfano saa 24, wiki au mwezi ambavyo hata kama mteja hakutumia simu muda huo ukishapita salio husika haliwezi kutumika tena.
One Comment
Comments are closed.