WhatsApp inazidi kuongeza vipengele ambavyo kwa namna moja au nyingine itazidi kulifanya kampuni na ushindani wa hali ya juu kwa makampuni mengine.
Sasa hivi tutegemee mtandao huo wa kijamii (WhatsApp)kuja na kipengele cha Community, lakini kipengele hichi ni kwa ajili ya makundi (Group) katika mtandao huo.
Community itakua inabeba makundi makubwa sana na pengine labda kwa yale makundi yenye mlolongo mrefu wa mahojiano.
Japokua mtandao wa WhatsApp haukuweka bayana mambo mengi hadharani, mambo kama ni nchi gani ambazo zitaanza pata huduma hii n.k.
Hapa kinachofanyika sio tofauti sana na ma’group (makundi) ya Facebook jinsi yalivyo, sasa kuwa na fikira hiyo hiyo yaaani mfumo huo wa makundi kuhamia katika mtandao huo.
Kwa sasa ni kwamba huduma hii iko katika hatua za maandalizi na kwa sasa imefikia mpaka katika hatua ya majaribio, pengine kipengele hichi kitaanza kupatikana hivi karibuni kwa watumiaji wote wa mtandao huu.
Kama mtu ni mmoja wapo katika wana’community ana uwezo wa kutoka au kutolewa na Admin kama ilivyo katika ma’Group ya kawaida tuu.
Mpaka sasa ma’Group hayo yana uwezo wa kufikisha hadi idadi ya watu 512 tuu lakini tunahisi idadi hii itaongezeka huko mbeleni.
licha ya mtandao huo kuzidi kufanya maboresho kadha wa kadha na kuongeza vipengele katika WhatsApp ya kawaida na ile WhatsApp Business bado kampuni inaendelea kuongeza vipengele vingine
Mpaka sasa mtandao huo haujatoa tamko juu ya lini kipengele hiki kitaanza kupatikana kwa watumiaji wote—hatuna budi kusubiri…
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika sehemu ya comment, je hili umelipokeaje? Unadhani ni sawa kabisa kuwa na sehemu ya makundi ambayo inajitegemea katika mtandao wa WhatsApp.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.