Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Facebook, Bw. Mark Zuckerberg amesema hivi karibuni WhatsApp Business itaanza kupatikana kwenye simu za mfumo wa iOS.
Mark Zuckerberg aliyasema hayo Katika Mkutano wa F8 ambapo alikuwa akielezea mafanikio ya WhatsApp Business katika makampuni madogo yalioanza kutumia programu hiyo huku moja ya mipango ni kuongeza zaidi watumiaji wa programu ya WhatsApp Business.
Aidha, njia ya kuongeza watumiaji wa WhatsApp Business ni kuanza kupatikana katika simu za mfumo wa iOS (simu za iPhone). Tangu kuanza kwa programu tumishi hiyo imekuwa kwa ajili ya simu za Android tu na mpaka sasa WhatsApp Business ina watumiaji zaidi ya milioni tatu duniani kote.
WhatsApp Business ni nini?
WhatsApp Business ni toleo maalum la WhatsApp kwa ajili ya makampuni na wafanyabiashara ambapo umesaidia sana makampuni na wafanyabiashara kutenganisha mazungumzo ya kawaida na yale yanayohusu biashara. Pia imesaidia kutangaza biashara na bidhaa mbalimbali za makampuni na wafanyabiashara. Kujua zaidi kuhusu WhatsApp Business BOFYA HAPA.
WhatsApp business ya kwenye iOS inamuwezesha mtumiaji kutuma ujumbe wa salamu kwa mteja aliyemtumia ujumbe kwa mara ya kwanza.
Programu tumishi ya WhatsApp Business kwenye iOS bado inafanyiwa kazi (ipo katika hatua za mwanzo kabisa) na kuna baadhi ya vipengele kama vile labels na Quick Replies bado havijaonekana kwenye programu hiyo lakini vipo kwenye WhatsApp Business upande wa Android.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.