Ni wazi karibia kila kitu kina tuzo zake siku hizi, tuzo zipo za aina nyingi sana huku kukiwa na zile tuzo ambazo zinaaminiwa kuwa ndio kubwa kushinda zote.
Kwa mfano katika muziki inaaminika kuwa tuzo kubwa kabisa ni Grammy na katika tasnia ya Filamu na Maigizo inaaminika kuwa ni zile tuzo za Oscar.
Vipi Kuhusu Ma’game’? tuzo hizi zinajulikana kama ‘The Game Awards’ na kwa mwaka huu ziatafanyika katika ukumbi wa Microsoft maarufu kama Microsoft Theater.
Wakati wa kutoa tuzo hizi kutakuwa na wahudhuriaji kabisa, tofauti na mwaka jana ambapo gonjwa la CORONA lilikua limeshamiri. Lakini hata hao watakaofanikiwa kuhudhuria ni wale wageni waalikwa tuu.
Ukaichana na kuwa tuzo hizi zitatolewa huku kukiwa kuna wageni waalikwa, pia zitaweza kurushwa mubashara na kurushwa kwa zaidi ya vituo 40 tofauti tofauti.
Vile vile ukiachana na tuzo zenyewe kutakuwa na michezo na mashindano ya aina mbalimbali ikiwa ni kama sehemu ya starehe na viburudisho kwa wahudhuriaji.
Kuna vitu vingi vitakua vikiwa vinafanyika, kama vile utambulisho wa ma’game’ mapya kwa mara ya kwanza. n.k.
Ningependa kusikia kutoka kwako, je na wewe napenda ma’game’? naomba nitajie ‘game’ lako unalolipenda zaidi ukiachana na lile la Nyoka😅
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Katika Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.