Utajiri unaweza kutokana na sababu mbalimbali na sasa mwanamziki wa miondoko ya RnB amejiongezea utajiri wake baada ya kulipwa karibu $1bn na Snapchat Inc. kutokana na kejeli!
“Mzaha mzaha hutumbua usaha” ni msemo ambao una maana kubwa katika kila jambo ambalo unaweza ukafikiri lisiwe na madhara makubwa lakini mwisho wa siku ukaishia kuingia gharama ambazo hukuzitarajia.
Rihanna ameshika vyombo vya habari duniani baada ya kuilalamikia Snapchat kwa kumtumia yeye pamoja na Chris Brown katika matangazo ya kwenye mtandao wa kijamii wa Snapchat; tangazo hilo liliuliza iwapo mtu “Angechagua kumchapa kibao Rihanna au kumpiga ngumi Chris Brown“.
Msanii huyo wa RnB aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kwamba tayari Snapchat wanajua kuwa huo sio mtandao wa kijamii anaoupenda na angeweza kulinyamazia jambo hilo la kejeli lakini ameamua kufanya hivyo kuwawakilisha wanawake, wanaume pamoja na wale wote ambao ameshawahi kutumiwa na makampuni mbalimbali kuwakejeli.
Snapchat waliomba msamaha kwa Rihanna na kudai kuwa tangazo hilo lilitoka kimakosa bila ya kupitiwa lakini mameno hayo hayakumshawishi msanii huyo kuweza kuisamehe kampuni hiyo na kuacha jambo hilo lipite tu.
Vyanzo: Telegraph, Today Fm
One Comment
Comments are closed.