Sio Apple tuu hata makampuni mengine mengi katika soko la simu janja duniani bado hajwajiingiza katika soko hili.
Inaamana soko la simu za kujikunja ni gumu au tatizo linakua ni nini, kwa haraka haraka tena kwa kiasi kikubwa ni kwamba kampuni ya Samsung inaonekana dhahiri kwamba imeliteka soko hili wakati Apple hawaonekani kabisa.
Hivyo yapaswa kusema katika simu janja za kujikunja wao ndio wameliteka soko, licha ya kuwa na ushindani mkubwa sana na Apple kwa miaka mingi tuu..
…Lakini bado Apple hawajajiingiza rasmi katika soko hilo, japokuwa kwa sasa kuna fununu nyingi kuwa kampuni iko katika hatua za kuhakikisha wanakuja na simu za kujikunja.
Kwa sasa kampuni ya Samsung na makampuni mengine mengi yanaendelea kuleta simu za kujikunja katika soko.
Kwa upande wa Samsung wao wana mpango wa kuuza simu za kujikunja kwa kiwango cha nusu tuu ya mauzo yao ya simu janja za kawaida kwa mwaka.
Vile vile kingine cha kufurahisha ni kwamba soko hili linazidi kukua kila kukicha maana hata watumaiji wa simu za aina hizi wanazidi kuongezeka.
Kwa makampuni mengi ni kwamba yanashindwa kuingia katika soko hili kwa kuwa ili kifaa (simu) moja itengenezwe huwa inachukua gharama nyingi ukilinganisha na simu janja za kawaida.
Kwa kampuni kama Apple, ni wazi kuwa inaweza kuendana kabisa na hizo gharama, kwa haraka haraka hapa ninachokiona ni kwamba kampuni imeamua kufuata ratiba zake tuu bila kusikiliza kwingine.
Pengine watatoa simu hiyo ya kujikunja kipindi ambapo wataona ni sawa wao kama wao japokua ndio hivyo tena wanachukua muda mrefu sana.
Lakini kuna kitu cha kukiweka akiliini pia, umeshawahi kufikiria pengine kampuni ya Apple inaweza isije kabisa na simu za aina hii (za kujikunja).
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment je hii umeipokeaje? Je unadhani ni sawa kwa Apple kujiingiza katika soko hili?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.