Kama makampuni ya Apple huwa ina tabia ya kutoa matoleo madogo –ki umbo–ya simu yenye uwezo mkubwa na kuyapa majina ya SE, Google Pixel na wenyewe wameona waje na kitu kama hichi.
Kwa sasa ni wazi kabisa kwamba katika soko simu za Google Pixel zinafanya vizuri sana na imekua ni moja kati ya simu ambazo zimeleta ushindani mkubwa katika soko la simu janja.
Lakini kwa dunia ya sasa hivi ni kwamba watu wengi hawapendelei kutumia simu ndogo (zenye vioo vidogo) pengine ndio sababu simu kubwa zinajichukulia nafasi za juu katika soko.
Vile vile kumbuka mwezi ujuo simu janja za Google Pixel 7 na Pixel 7 Pro ukiachana na watu kuwa na shauku kubwa juu ya matoleo haya mawili ya simu bado kampuni ina mpango wa kuja na simu ndogo.
Kinachofanyika hapa ni kwamba kampuni itakuja na simu yenye umbo dogo lakini ikiwa na sifa (specification) za hali ya juu.
Lakani hii itakua ni mahususi kwa wale ambao hawapendelei simu kubwa kubwa, kubuka kuona simu ya Pixel yenye umbo dogo ni mwaka 2020.
Kwa sasa simu hiyo imepewa jina la utani, jina hilo ni ‘Neila’ na mpaka sasa bado haijajulikana kwamba simu hiyo ina sifa gani za undani.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je uko tayari kuanza kutumia Google Pixel yenye umbo dogo?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.