Jambo la kufuta picha/video ni kitu ambacho kimezoeleka na huwenda mtu anakuwa amefuta kwa bahati mbaya au akiwa amekusudia kuzifua. Imethibitika kuwa inawezekana kurudisha picha au video ambazo zimefutwa kwenye simu janja yako.
Kuweza kurudisha vitu vilivyofutwa kwenye simu janja si jambo rahisi lakini pia linahitaji umakini mkubwa wakati wa kufanya jitihada kuweza kurudisha data zako kwenye simu.Hatua za kufuta wakati wa kurudisha vitu vilivyofutwa kwenye simu janja:-
- Pakua Android Data Recovery. App hii ndio itakayokuwezesha kurudisha picha/video ambazo zilikuwa zimefutwa. Pakua hapa kwa wenye kutumia Windows OS na bofya hapa>>iOS kwa wanaotumia kompyuta za Mac. Baada ya kuipakua app hii unganisha simu yako kwenye kompyuta kwa kutumia USB.
- Ruhusu ‘USB debugging’. Hatua hii ya pili itawezesha simu yako iweze kufanya kile ambacho unakikusudia kwa msaada wa app hii, Ingia Settings>>Developer Options>>USB debugging. Bofya ok baada ya USB debugging kufunguka.
- Kuchagua mafaili ya kurudisha. Baada ya simu yako kutambukiwa kwenye kompyuta, programu hii maalum itakuleta kwenye ukurasa ambao utakuruhusu kuchaguadata unazotaka kurudisha.
Baada ya data kuwa zimeshasafishwa; kwanye simu janja yako kitatokea kiboksi ambacho utakakiwa kubonyeza “Allow” na kama hakitatokea basi bofya “Retry“.
- Kurudisha data. Hii itakuwa ndio hatua ya mwisho. Baada ya mchakato mzima wa kusafisha data zilizofutwa (picha, video, sms, n.k) itakubidi uchague vile unavyotaka kurudisha na baada ya hapo utabofya “Recover“.
Daima ni muhimu kuwa makini sana pale tunapotumia simu zetu ili kuepuka kufuta vitu muhimu kwenye simu zetu. Usiwe na shakaiwapo umefuta sms kwenye simu yako; bofya hapa kujua zaidi.
Vyanzo: RecoveryAndroid, mitandao mbalimbali
One Comment
Comments are closed.