iPhone X ndio simu pekee ambayo bado haijanza kuuzwa ingawa tayari imekwishazinduliwa pamoja simu janja nyingine kutoka Apple. Bw. Steve Wozniak amesema hatonunua simu hiyo mara tu zitakapoanza kuuzwa kutokana na kutomvutia.
Kwa wasio fahamu, Bw. Steve Wozniak ndiye mwanzilishi mwenza (baada ya marehemu Steve Jobs) wa kampuni ambayo mpaka hivi leo inasifika sana katika biashara ya vifaa vya kiteknolojia (simu, saa, kompyuta, n.k).
Uamuzi wa Bw. Steve Wozniak umekuja baada ya kuona simu janja ya iPhone X haina tofauti kubwa na iPhone 8 hivyo haoni sababu ya kumiliki iPhone X mara tu zitakapoanza kuuzwa mnamo Novemba 3 (unaweza kuanza kuagiza kuanzia Oktoba 27 2017).
Historia fupi ya Bw. Steve Wozniak na Apple kwa ujumla.
Apple (kampuni) ilianzishwa mwaka 1976 na Bw. Wozniak na Steve Jobs. Wawili hao walishirikiana bega kwa bega katika uundaji wa vifaa vya kiteknolojia na kuifanya Apple kuwa na jina na kuwa moja ya kampuni bora zaidi kwenye masuala ya kiteknolojia.
Bw. Wozniak alihusika sana kwenye uundaji wa bidhaa husika za mwanzo kabisa za wakati huo huku marehemu Jobs yeye akiwa na uono wa mbali wa bidhaa husika kuwa itafanya vyema pamoja na kuitangaza bidhaa yenyewe.
Mwaka 1985, Bw. Wozniak aliachana na Apple baada ya kutopendezwa na mwenendo wa kampuni kwa wakati huo lakini amekuwa mmoja ya watu ambao wananunua bidhaa za Apple mara tu zinapotoka. Kujua mengineyo kuhusu Bw. Steve Wozniak BOFYA HAPA!
Mwanzilishi huyo mwenza wa Apple ana amini kuwa simu janja nyingi za siku hizi zimekosa msisimko kama ilivyokuwa zamani kutokana na simu hizo kuwa na tofauti ndogo mathalani yeye (Wozniak) anaona iPhone 8 ipo sawa na iPhone 7, iPhone 6 😯 😯 .
HIvi sasa si shabiki sana wa simu janja kama miaka ya nyuma na anaangazia zaidi teknolojia za ndege zinajiendesha zenyewe, magari yanayotumia nishati ya umeme, magari yanayojiendesha yenyewe na wanachofanya kampuni hizo.
Vyanzo: NBC, Telegraph