Electronic Arts au maarufu kama EA ni kampuni nguli inayojishughulisha na utengenezaji wa michezo (Game) ya aina mbali mbali.
Baadhi ya michezo maarufu ni kama FIFA, Madden, Battlefield na Need for Speed ambayo yote inaandaliwa na kampuni hiyo.
Habari zilipotoka kuwa kampuni hiyo iko sokoni au kama kuna uwezekano wa kujiunga na kampuni nyingine zilipotoka ziliwashtua wengi.
Mpaka sasa makampuni ambayo yanahisiwa yanaweza kuinunua kampuni hiyo au kukubali muungano ni kama Apple, Disney, Amazon, NBCUniversal na mengine mengi tuu.
Kwa makampuni makubwa kama haya mara nyingi muungano na kampuni tajiri kuzidi inakuaga ni kitu kuzuri zaidi kuliko kuuzwa kabisa
Kumbuka ukiungana kuna vitu vingi vinabaki kama kawadia mfano sehemu ya wafanyakazi na mara nyini mwenendo wa bishara jini ulivyokua.
Mpaka sasa haijaulikana dhahiri kuwa ni nani atanunua au kuungana na kampuni hiyo, ila kama kawaida taarifa zikitoka lazima tutakuandikia hapa hapa TeknoKona.
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Comment, Hii Umeipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.