Makampuni kadha wa kadha isipokuwa Apple wamejitahidi kuhakikisha bidhaa zao zinapata masasisho (kuhamia) kwenye Android 9 ili kuweza kupata kuona kile ambacho kimeboreshwa.
NOkia wameweka wazi ratiba ya simu zao ambazo mpaka sasa zinafika matoleo kumi na tano kwa idadi; 5 kati ya hizozikiwa tayari zimesharuhusiwa kuweza kupakua programu endeshi toleo la kenda na matoleo mawili mengine mpango wa kuruhusu kuweza kushisha ukiwa unaendelea.
Tayari Nokia 5.1 Plus, 6.1, 6.1 Plus, 7 na 7.1 Plus zimepewa kibali cha kupokea/kuweza kuhamia Android Pie. Huku kwa Nokia 8 na 8 Sirocco zikiwa kwenye mchakato wa kuweza kuruhusiwa kupokea masasisho hayo.
Orodha na lini simu za Nokoa zitapokea masasisho ya Android 9
Simu
Ruhusa ya kuweza kupakua Android 9
Nokia 3.1 Plus Januari 2019 Nokia 5 Januari 2019 Nokia 2.1 Kwenye robo ya kwanza ya mwaka 2019 Nokia 3.1 Kwenye robo ya kwanza ya mwaka 2019 Nokia 5.1 Kwenye robo ya kwanza ya mwaka 2019 Nokia 6 Kwenye robo ya kwanza ya mwaka 2019 Nokia 1 Mwanzoni mwa robo ya pili ya mwaka 2019
Nokia 3 Mwanzoni mwa robo ya pili ya mwaka 2019
Kama unatumia Nokia 2 basi itakubidi usubiri haijulikani mpaka lini ili kuweza kushusha Android 9 kwani haipo kwenye orodha ya simu za Nokia ambazo zitaweza kushusha toleo hilo la programu endeshi.
Vipi Nokia unayotumia ipo kwenye mpango au tayari umeshahamia kwenye Android kenda?
Vyanzo: Android Authority, The Verge