Moja ya watu kukimbilia simu janja zenye uwezo mkubwa ni mapenzi yao kwa magemu ambapo inatumika kama kiburudisho kama namna moja ya kuchangamsha ubongo.
Kwa wengi wetu ambao tunapenda kucheza magemu naamini kabisa tutakuwa tunafahamu gemu la magari-Rocket League ambalo sitapenda kulielezea zaidi lakini kuna habari njema. Gemu hilo linakwenda kuboreshwa na kuanzia Mei 20 ya mwaka huu yale magari ya mbio za langalanga yatapatikana humo.
Magari ya mbio za langalanga kwenye gemu la Rocket league
Mbio za lanagalanga ni yale mashindano ya magari maarufu sana duniani ambayo yanajulikana kama “Formula One (F1)” kwa Kiingereza. Sasa gemu la Rocket League litakuwa na magari mbio za langalanga, madereva ambapo kwa mtu kuweza kuendesha ingizo hilo jipya la magari hayo itamgarimu pointi 2000 au kati ya $18-$20.
Mbali na ujio wa magari hayo pia mchezaji ataweza kupata uwezo wa kutumia gari lambio za langalanga mwaka 2021. Pia, yatakuwepo mashindano mengine yakihusisha timu nyingine kama McLaren, Honda kama njia ya kuongeza chachu kwenye gemu hilo.
Kuna tofauti kati ya kuonekana ma kuweza kutumika
Magari hato ya mbio za langalanga yataingizwa kwenye genu husika Mei 20 ya mwaka 2021 lakini kuhusu mtu kuweza kuyatumia ni mpaka Mei 26 ikimgharimu mhusikakiasi cha pointi ama fedha zilizozitaja hapo awali.
Nina imani wapenzi wa gemu hili watakuwa wamefurahishwa na habari hii, si ndio? Ewe msomaji wetu usisahau kutembela tovuti ywtu kila siku ili kuweza kuhabarika kwenye masuala ya teknolojia.
Vyanzo: Engadget, Tovuti ya Rocket League
No Comment! Be the first one.